TEMBELEA KILA WIKI, SOMA HABARI MPYA. USIKOSE MENGI MENGINEYO WIKI IJAYO. TUPO MAHIRI KUKUHABARISHA PATA VITU VIPYA HAPA. PATA BURUDANI ,HADITHI NA MATUKIO YA MICHEZO KILA JUMA.

Uwanja wa taifa unaongoza kwa ukubwa nchini

Uwanja mkubwa kuliko vyote hapa nchini ni Uwanja wa Taifa ambao una uwezo wa kuchukua watazamaji 60,000.
Uwanja huu unamilikiwa na Serikali ya Tanzania ulijengwa kwa ushirikiano na serikali ya China mwaka 2007.
      
Ni moja kati ya viwanja bora barani Afrika ukiwa sawa na uwanja wa Kasarani wa Mathare Kenya ambao nao una uwezo wa kuchukua watazamaji 60,000.

Tangu uzinguliwe mwaka uwanja huu umechezwa na timu maarufu kama vile timu ya taifa ya Brazil, Cameroun, Ivory Coast na nchi za Afrika Mashariki na Kati.
     
Uwanja wa Jamhuri Morogoro

Uwanja wa Jamhuri Morogoro uko mkoa wa Morogoro unamilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM).

Uwanja huu ulijengwa mwaka 1978, una uwezo wa kuchukua watazamaji 20,000.
     

Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine

Uwanja wa Sokoine upo katikati ya jiji la Mbeya mwaka 1977, una uwezo wa kuchukua watazamaji 20,000 na unamilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM).

Wakati uwanja huu unazinduliwa rasmi mwaka 1977 ulipewa jina la uwanja wa Mapinduzi kutokana na mwaka huo kuwa ndiyo CCM ilizaliwa rasmi baada ya kuvunjwa kwa Chama cha Tanganyika African National Union (TANU).

Jina la uwanja wa Mapinduzi lilibadilishwa na kuitwa na luitwa kumbukumbu ya Sokoine kwa heshima ya Waziri Mkuu, Edward Moringe Sokoine aliyefariki kwa ajili ya gari  mkoani Morogoro akitokea Bungeni Dodoma.
         
Uwanja wa Jamhuri Dodoma

Uwanja wa Jamhuri upo katikati ya jiji la Dodoma unamilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM).

Uwanja huu ulijengwa mwaka 1978 una uwezo wa kuchukua watazamaji 20,000.
     
Uwanja wa Majimaji

Uwanja wa Majimaji upo katikati ya mji wa Songea mkoa wa Ruvuma unamilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM).

Uwanja huu una uwezo wa kuchukua watazamaji 30,000, unamilikiwa na Chama cha Mapinduzi, ulijengwa mwaka 1979.
    
Uwanja wa Mwanakalenge

Uwanja wa Mwanakalenge upo katika makao makuu ya Mkoa wa Pwani, Kibaha.

Uwanja huu ulijengwa mwaka 1979 na Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha una uwezo wa kuchukua watazamaji 5,000.
 
Uwanja wa Kirumba

Uwanja wa Kirumba upo jijini Mwanza unamilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM).

Uwanja huu ulijengwa mwaka 1980, una uwezo wa kuchukua watazamaji 45,000.

Kirumba ni uwanja wa pili kwa ukubwa Tanzania Bara.
 
Uwanja wa Lake Tanganyika 

Uwanja wa Lake Tanganyika upo Kigoma mjini unamilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM).

Uwanja huu ulijengwa mwaka 1980 una uwezo wa kuchukua watazamaji 15,000.
   
Uwanja wa Kambarage

Uwanja wa Kambarage upo Shinyanga mjini unamilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM).

Uwanja huu ulijengwa mwaka 1983, una uwezo wa kuchukua watazamaji 30,000.

Zamani uwanja huu ulijulikana kwa jina la uwanja wa Mwadui ulijengwa na kampuni ya Williamson Diamond iliyokuwa ikichimbaolmasi.
    
Uwanja wa Namfua

Uwanja wa Namfua upo katikati ya mji wa Singida unamilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM).

Uwanja huu uliejngwa mwaka 1982 una uwezo wa kuchukua watazamaji 10,000.
  
Uwanja wa Nyamagana

Uwanja wa Nyamagana ni moja kati ya viwanja vikongwe hapa nchini ulijengwa mwaka 1945.

Uwanja huu ulijengwa mwaka 1945 unamilikiwa na Halmashauri ya Jiji la Mwanza na una uwezo wa kuchukua watazamaji 15,000.
  
Uwanja wa Ilulu

Uwanja wa Ilulu upo katika mkoa wa Lindi unamilikiwa na Halmashauri ya Mkoa wa Lindi.

Uwanja huu ulijengwa mwaka 1957, una uwezo wa kuchukua watazamaji 10,000.
  
Uwanja wa Sheikh Amri Abeid

Uwanja wa Sheikh Amri Abeid upo katikati ya jiji la Arusha ambalo ni kitovu  cha utalii hapa nchini.

Uwanja huu ulijengwa mwaka 1957, unamilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM). Una uwezo wa kuingiza watazamaji 25,000.
   

Uwanja wa Karume

Uwanja wa Karume upo katika jiji la Dar es Salaam unamilikiwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Uwanja huu ulijengwa mwaka 1940, ndio uwanja mkongwe nchini kuliko viwanja vyote. Una uwezo wa kuchukua watazamaji 10,000.
  
Uwanja wa Uhuru

Uwanja wa Uhuru upo katika jiji la Dar es Salaam unamilikiwa na serikali.

Uwanja huu ulijengwa mwaka 1961 kwa madhumuni ya sherehe za uhuru wa Tanganyika.

Wakati unajengwa ulikuwa na uwezo wa kuchukua watazamaji 10,000 na ulipofanyiwa ukarabati wa kwanza uliongeza idadi ya watu na kufikia 15,000.

Kwa sasa uwanja huu unachukua watazamaji 30,000 na bado upo katika ukarabati.
    
Uwanja wa Kaunda

Uwanja wa Kaunda katika kitongoji cha Kariakoo eneo la Jangwani yalipo Makao Makuu ya klabu ya Young Africans Sports Club (Yanga).

Uwanja huu unamilikiwa na klabu hiyo ambayo ni ya kwanza nchini kujenga uwanja wake mwaka 1968, una uwezo wa kuchukua watazamaji 15,000.
   

Uwanja wa Memorial

Uwanja wa Memorial ni moja kati ya viwanja viwili vilivyoko katika mkoa wa Kilimanjaro umejengwa katikati ya mji huo na unamilikiwa na Halmashauri ya mji wa Moshi.

Uwanja huo ulijengwa mwaka 1957 una uwezo wa kuchukua watazamaji 15,000. Kwa miaka mingi uwanja huu hautumiki kwa shughuli yoyote.
         

Uwanja wa Mkwakwani

Uwanja wa Mkwakwani upo Mkoa wa Tanga unamilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM), ulijengwa mwaka 1972 na unachukua watazamaji 15,000.
      
Uwanja wa Samora

Uwanja wa Samora ulijengwa mwaka 1975, unamilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM), uwanja huu unachukua watazamaji wapatao 25,000.
         
Uwanja wa Kaitaba

Uwanja wa Kaitaba upo katika mkoa wa Kagera kando ya Ziwa Victoria ni mali ya Chama cha Mapinduzi (CCM). Ulijengwa mwaka 1976 unachukua watazamaji25,000
       

Uwanja wa Azam

Uwanja wa Azam unamilikiwa na klabu ya Azam ya jijini Dar es Salaam upo katika maeneo ya Chamazi nje kidogo ya jiji. Uwanja huu ulijengwa mwaka 2010 unachukua watazamaji 5,000, kwa sasa bado upo katika matengenezo.
    
Uwanja wa Nangwanda Sijaona

Uwanja wa Nangwanda Sijaona upo katika mkoa wa Mtwara ulijengwa mwaka 1992 na Halmashari ya mji wa Mtwara, unachukua watazamaji 10,000.
  
Uwanja wa Mgambo

Uwanja wa Mgambo upo katika wilaya ya Mpwapwani mkoa wa Dodoma mwaka 1972, ukiwa na uwezo wa kuchukua watazamaji 10,000.
  
Uwanja wa Mandela

Uwanja wa Mandela upo katika mkoa wa Rukwa unamilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM), unachukua watazamaji 15,000.
   
Uwanja wa Karume

Uwanja wa Karume upo katika mkoa wa Morogoro ulijengwa mwaka 1986 na Chama cha Mapinduzi (CCM), unachukua watazamaji 15,000.
  
Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi

Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi ulijengwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) mwaka 1988 unachukua watazamaji 30,000.
  
Uwanja wa Ushirika

Uwanja wa Ushirika upo mjini Moshi ulijengwa mwaka 1989 na Jumuiya ya Washirika (MUCCOS) una uwezo wa kuchukua watazamaji 10,000.
    
Uwanja wa Manungu

Uwanja wa Manungu upo Turiani Mkoa wa Morogoro ulijengwa mwaka 1999 na kampuni ya Mtibwa Sugar, unachukua watazamaji 10,000.
  
Uwanja wa Kahama Shinyanga 2002 Halmashauri 15,000

Uwanja wa Kahama upo katika wilaya ya Kahama mkoa wa Shinyanga ulijengwa mwaka 2002 unamilikiwa na Halmashauri ya mji wa Kahama, unachukua watazamaji 15,000.
      

2005 - Fainali za Vijana Afrika

Tanzania ilipata nafasi ya kucheza fainali za Vijana Afrika nchini Mali mwaka 2005, lakini kwa bahati mbaya, Shirikisho la Soka Afrika (CAF) liliinyang'anya Tanzania nafasi hiyo baada ya kubainika kuwa ilimchezesha ilipoteza Nurdin Bakari ambaye alibaini kudanyanga umri.
Nafasi ya Tanzania ilipewa Zimbabwe.

   

Fainali za Mataifa Afrika

Tanzania imeshiriki fainali moja ya kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 1980. Kwani mwaka 1992 ilitolewa hatua za awali, 1998 ilijitoa, 2004 ilijitoa 2006, 2008, 2010 ilitolewa hatua za awali.
     

Tanzania na CAF

Tanzania ilijiunga  na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) mwaka 1960.
      

Je wajua

 Soka Afrika Mashariki

Nchi za Afrika Mashariki Tanzania, Kenya na Uganda zilianza mchezo wa soka mwanzoni mwa mwaka 1920 baada ya Waingereza kuingia Afrika Mashariki wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia 1914 na Vita Kuu ya Pili 1945.
           

kodi za ubingwa

1965 Sunderland (Simba SC)
1966 Sunderland
1967 Cosmopolitan
1968 Young Africans
1969 Young Africans
1970 Young Africans
1971 Young Africans
1972 Young Africans
1973 Simba SC
1974 Young Africans
1975 Mseto SC
1976 Simba SC
1977 Simba SC
1978 Simba SC
1979 Simba SC
1980 Simba SC
1981 Young Africans
1982 Pan Africans
1983 Young Africans
1984 KMKM
1985 Young Africans
1986 Tukuyu Stars
1987 Young Africans
1988 Coastal Union
1989 Young Africans
1990 Simba SC
1991 Young Africans
1992 Young Africans
1993 Young Africans
1994 Simba SC
1995 Simba SC
1996 Young Africans
1997 Young Africans
1998 Young Africans
1999 Prisons
2000 Mtibwa Sugar
2001 Simba SC
2002 Young Africans
2003 Simba SC
2004 Simba SC
2005 Young Africans
2006 Young Africans
2007 Simba SC
2007/08 Young Africans
2008/09 Young Africans
2009/2010 Simba SC
2010/2011 Young Africans

 
Wafungaji na matokeo ya mechi za Simba na Yanga 1965 hadi 2008 Ubingwa wa Tanzania
tangu kuanza mashindano hayo mwaka 1965.

1965:Sunderland (Simba)
Matokeo Sunderland 1 Yanga 0
Mfungaji Mawazo Shomari dk 15.

1966:Sunderland
Matokeo Sunderland 3 Yanga 2
Wafungaji Sunderland: Mustafa Choteka dk 24, Haji Leso dk 86, Emmanuel Albert dk 83.
Wafungaji Yanga: Abdulrahim Lukongo dk 54, Andrew Tematema dk 67.

1967:Hazikucheza

1968:
Matokeo Yanga 5 Sunderland 0
Wafungaji:Maulid Dilunga dk 18,43, Salehe Zimbwe dk 54,89, Kitwana Manara dk 86.

1969: Hazikucheza

1970: 
Yanga 1 Sunderland 0 Mfungaji Maulid Dilunga

1971:
Sunderland 1 Yanga 2
Wafungaji
Sunderland Omar Gumbo
Yanga Fred Mayaula Mayoni-2

1972:
Sunderland 0 Yanga 1
Mfungaji Leonard Chitete dk 12
Mpira ulivunjika dakika 19 kipindi cha pili baada ya Willy Mwaijibe kupigwa kiwiko na Kitwana Manara na FAT kuitangaza Yanga bingwa.

1973:
Simba 1 Yanga 0
Mfungaji Haidari Abeid dk 66

1974:
Yanga 2 Simba 1
Wafungaji
Simba Adam Sabu dk 16
Yanga Gibson Sembuli dk 87,Sunday Manara dk 97

1975: Hazikucheza

1976:  Hazikucheza
Yanga ilisambaratika na wachezaji wake wa kikosi cha kwanza kujiunga na Nyota Afrika ya Morogoro ambayo ilicheza fainali na Simba na matokeo Simba 1 Nyota 0 mfungaji wa goli la Simba Abbas Dilunga dk 82.

1977:
Simba 6 Yanga 0
Wafungaji Kibaden dk 10, 42, 89, Jumanne Masimenti dk 60, 73 na Selemani Saidi wa Yanga kujifunga dk 20.

1978: Hazikucheza
Ilicheza fainali ya Pamba ya Mwanza na kushinda 2-1 wafungaji Jumanne Masimenti na Willy Mwaijibe.

1979:
Simba 3 Yanga 1
Wafungaji Simba Nicco Njohole dk 3, Mohamed Tall dk 36, Abbas Dilunga dk 72.
Yanga Rashid Hanzuruni dk 38.

1980:
Simba 3 Yanga 0
Wafungaji Simba: Abdallah Mwinyimkuu dk 29, Thuwein Ally dk 82 na Nicco Njohole dk 83.

1981:
Simba 0 Yanga 1
Mfungaji Juma Mkambi dk 42

1982:
Simba 0 Yanga 0
Marudiano:Simba 0 Yanga 3
Wafungaji: Omary Hussein dk 2,86, Makumbi Juma dk 62
 
1983:
Simba 1 Yanga 3
Wafungaji Yanga: Charles Boniface dk 21,Makumbi Juma dk 38, Omary Hussein dk 84
Simba  Kihwelu Mussa dk 14.
Marudiano Simba 1 Yanga 1 
Wafungaji
Simba Lilla Shomari dk 72
Yanga Ahmad Amasha dk 89

1984: 
Simba 1 Yanga 1
Wafungaji
Simba Idd Pazi dk 20
Yanga Omary Hussein dk 72
Marudiano: Simba 1 Yanga 1
Simba Zamoyoni Mogellah dk 17
Yanga Abeid Mziba dk 39

1985:
Simba 1 Yanga 1
Wafungaji
Simba Mohamed Bob Chopa dk 30
Omary Hussein dk 6
Marudiano Yanga 2 Simba 1

1986:
Simba 1 Yanga 1
Wafungaji
Simba John Douglas dk 20
Yanga Abeid Mziba dk 22.
Marudiano: Simba 2 Yanga 1
Wafungaji: Simba Edward Chumila dk 9 Malota Soma dk 51 Yanga Omary Hussein dk 5

1987:
Yanga 1 Simba 0
Mfungaji Edgar Fongo dk 36
Marudiano: Simba 0 Yanga 1
Mfungaji Abeid Mziba dk 14

1988:
Simba 1 Yanga 1
Wafungaji
Simba Edward Chumila dk 25
Yanga Justin Mtekele dk 28
Marudiano: Simba 2 Yanga 1
Wafungaji Simba Edward Chumila dk 21 John Makelele dk 85 Yanga Issa Athumani dk 36

1989:
Simba 1 Yanga 2
Wafungaji Simba Malota Soma dk 30
Yanga Issa Athumani dk 4 Abeid Mziba dk 85.
Marudiano: Simba 0 Yanga 0

1990:
Simba 1 Yanga 0
Mfungaji Mavumbi Omary dk 6
Marudiano: Simba 1 Yanga 3
Wafungaji Simba Edward Chumila dk 58
Yanga Makumbi Juma dk 33 Thomas Kipese dk 62, Sanifu Lazaro dk 89

1991
Ligi ya Tanzania Bara Simba 0 Yanga 1
Mfungaji Saidi Swedi Scud dk 7
Marudiano: Yanga 1 Simba 0
Mfungaji Saidi Swedi Scud dk 33
Ligi ya Muungano Simba 0 Yanga 2
Wafungaji Athumani China dk 8, Abubakary Salum 'Sure Boy dk 54
Marudiano: Simba 0 Yanga 2
Mfungaji Saidi Mwamba Kizota dk 41,72

1992:
Ligi ya Tanzania Bara Yanga 1 Simba 0
Mfungaji Kenneth Mkapa dk 10
1993: Bingwa Simba

1994: Ligi ya Tanzania Bara Yanga 2 Simba 0
Wafungaji Mohamed Hussein, James Tungaraza
Marudiano: Simba 4 Yanga 1 (George Masatu, Athumani China, Madaraka Selemani, Dua Saidi. Yanga Constantine Kimanda.
Ligi ya Muungano
Simba: 1 Yanga 0 Madaraka Selemani
Simba: 2 Yanga 0 George Lucas, Madaraka Selemani

1995
Simba 0 Yanga 0
Simba 2 Yanga 1
Wafungaji: Simba Saidi Mwamba Kizota dk 70, Mchunga Bakari dk 79
Yanga Mohamed Hussein Mmachinga dk 40.

1996
 Simba 0 Yanga 2
Simba 0 Yanga 0
Ligi ya Muungano
Simba 0 Yanga 1
Mfungaji Mohamed Hussein dk 46
Simba 4 Yanga 4
Wafungaji Simba: Thomas Kipese dk 7, Ahmad Mwinyimkuu dk 43, Dua Saidi dk 60, 90.
Yanga: Edibilu Lunyamila dk 28, Mustapha Hoza kujifunga dk 54, Saidi Mwamba dk 70 na Sanifu Lazaro dk 75

1997
Simba 1 Yanga 1
Wafungaji Simba Abdallah Msamba dk 1
Yanga Idelphonce Amlima dk 16
Simba 0 Yanga 0
 Simba 1 Yanga 1
Ligi ya Muungano
Wafungaji Simba George Masatu dk 89
Yanga Sekilojo Chambua dk 52
Simba 0 Yanga 1
Sekilojo Chambua dk 85

1998
Simba 1 Yanga 1
Wafungaji Simba Athumani Machepe dk 88
Yanga Akida Makunda dk 48
Simba 1 Yanga 1
Wafungaji Simba Abuu Juma dk 32
Yanga Idelphonce Amlima dk 28.

1999
Simba 1 Yanga 3
Wafungaji Simba Juma Amiri Maftaha dk 12
Yanga: Idd Moshi dk 59, Kalimangonga Ongara dk 64, Salvatory Edward dk 70
Simba 0 Yanga 2
Wafungaji Bakari Malima dk 49, Mohamed Hussein dk 71

2000:
 Nane Bora
Juni 25,2000 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam
Simba 2 Yanga 1 Stephen Mapunda-2 dk 59,70 Yanga Idd Moshi dk 5
Marudiano
Agosti 5, 2000 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam
Yanga 2 Simba 0 Idd Moshi dk 36,47


2001:
Nane Bora
Septemba 1,2001 CCM Kirumba Mwanza
Simba: 1 Yanga 0 Joseph Kaniki dk 75
Marudiano
Septemba 30,2001 CCM Kirumba Mwanza
Simba: 1 Yanga 1 Joseph Kaniki dk 65, Yanga Sekilojo hambua dk 87
2002: Bingwa Simba
Nane Bora
Agosti 18,2002 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam
Simba: 1 Yanga 1 Madaraka Selemani dk 67, Yanga Sekilojo Chambua dk 86
Marudiano
Novemba 10 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam
Simba 0 Yanga 0

2003
 Nane Bora
Septemba 28,2002 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam
Simba 2 Yanga 2 Emmanuel Gabriel dk 26,35 ,Yanga Kudra Omary dk 42, Herry Morris dk 58.
Marudiano
Novemba 2,2003 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam
Simba 0 Yanga 0

2004
Nane Bora
Agosti 7,2004 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam
Simba 2 Yanga 1 Shabani Kisiga dk , Ulimboka Mwakingwe , Yanga Pitchou Kongo
Marudiano
Septemba 18,2004 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam
Simba 1 Yanga 0 (Athumani Machupa dk 82)

2005
Ligi Kuu Bara
Aprili 27,2005 Uwanja wa Jamhuri Morogoro
Simba 2 Yanga 1 Nurdin Msiga dk 44, Athumani Machupa dk 63, Yanga Aaron Nyanda dk 39.
Marudiano
Agosti 21,2005 Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha
Simba 2 Yanga 0 Nicco Nyagawa dk 22,dk 57

2006 Bingwa Yanga
Ligi Kuu Bara
Machi 26,2006 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam
Simba 0 Yanga 0
Marudiano
Oktoba 29,2006 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam
Simba 0 Yanga 0

2007
Fainali ya Ligi Ndogo Bara
Julai 8, 2007 Uwanja wa Jamhuri Morogoro
Simba 1 Yanga 1 Moses Odhiambo dk 2, Yanga Saidi Maulid dk 65
Penalti Simba 4 Yanga 3 Saidi Swedi, Nicco Nyagawa, George Owino, Haruna Moshi (Waliokosa Shabani Kisiga, Moses Odhiambo
Yanga (Wisdom Ndlovu,Amri Kiemba, Thomas Maurice
Waliokosa Shadrack Nsajigwa, Abdul Mtiro, Abdi Kassim, Mrisho Ngasa
Marudiano
Oktoba 24,2007 Uwanja wa Jamhuri Morogoro
Simba 1 Yanga 0 (Ulimboka Mwakingwe dk 30)
Marudiano
Aprili 27, 2008 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam
Simba 0 Yanga 0
2008 Ligi kuu Bara
Oktoba 26,2008
Simba 0 Yanga 1
Mfungaji Ben Mwalala dk 16
Marudio Aprili 26, 2009
Simba 2 Yanga 2
Wafungaji Simba Ramadhan Chombo 'Redondo dk Haruna Moshi Boban dk
 Yanga Ben Mwalala dk  Jerry Tegete dk

1998- Majimaji bingwa Tanzania

Majimaji ya Songea mkoa wa Ruvuma ilifanikiwa kuchukua ubingwa wa Ligi ya Muungano mwaka 1998.

1999- Prisons yachukua ubingwa mara ya kwanza

Timu ya Tanzania Prisons ni moja kati ya timu kongwe hapa nchini ilianza kuingia katika ligi ya Dar es Salaam tokea miaka ya sitini.

Prisons inamilikiwa na Jeshi la Magereza pamoja na ukongwe wake imefanikiwa mara moja kuchukua ubingwa wa Tanzania ikiwa na mastani yake Mbeya badala ya Dar es Salaam.