Historia ya klabu bingwa ya Tanzania inaonyesha kuwa vigogo vya Yanga na Simba ndivyo vinavyoongoza katika kuchukua ubingwa wa Tanzania kwa nyakati tofauti.
Vigogo hivi vimekuwa vikipokezana kombe hilo tangu kuanzishwa mwaka 1965. Timu iliyofuatia mbali ya timu hizi mbili ni Cosmopolitans mwaka 1967 ilichukua taji hilo.
Hata hivyo, wakati Super League inaanzishwa rasmi mwaka 1992, Pan Africans ya jijini Dar es Salaam ndiyo iliyochukua ubingwa huo na hivyo kuwa timu ya pili kulipapata taji hilo ukiziondoa timu za Simba na Yanga.