TEMBELEA KILA WIKI, SOMA HABARI MPYA. USIKOSE MENGI MENGINEYO WIKI IJAYO. TUPO MAHIRI KUKUHABARISHA PATA VITU VIPYA HAPA. PATA BURUDANI ,HADITHI NA MATUKIO YA MICHEZO KILA JUMA.

Julai 20,1977- Kibaden apiga Hat-trick Yanga

Katika historia ya mapambano ya mahasimu wa jadi timu za Simba na Yanga, mchezaji aliyeweka rekodi ya kufunga magoli matatu katika mechi za mahasimu hao ni Abdallah 'King' Kibaden (Chief Mputa).


Kibaden aliweka rekodi hiyo katika mechi iliyochezwa Julai 20, 1977 kwenye uwanja wa Taifa (Uhuru).

Simba ilishinda 6-0, Kibaden alifunga magoli matatu  dakika ya 25,40,44.

Abdallah Kibaden (katikati) akiwa katika benchi la wachezaji wa Simba katika moja ya mechi za timu hiyo miaka ya 90. Kulia ni Kocha Msaidizi Etinne Eshete na kushoto ni Daktari Msemakweli