TEMBELEA KILA WIKI, SOMA HABARI MPYA. USIKOSE MENGI MENGINEYO WIKI IJAYO. TUPO MAHIRI KUKUHABARISHA PATA VITU VIPYA HAPA. PATA BURUDANI ,HADITHI NA MATUKIO YA MICHEZO KILA JUMA.

1970- Dilunga atinga na suti uwanjani

Mshambuliaji anayeminika kuwa kuwa ndiye nyota wa jezi namba 10 hapa nchini katika miaka ya 70, Maulid Dilunga wa Yanga alifanya kejeli dhidi ya mahasimu wao wa jadi Simba.

Dilunga alifunga goli kabla ya mapumziko katika mechi ya fainali ya klabu bingwa dhidi ya Simba ambapo matokeo hadi mapumziko yalikuwa Yanga 1-0.

Dilunga hakurudi uwanjani kipindi cha pili, badala yake alikwenda nyumbani kwa muda, kishaaliporejea uwanjani alikuwa amebadili mavazi na kuvaa suti.  Mpira ulipomalizika, Yanga ilishinda 1-0.